TRENDING POSTS

John Magufuli: Utayakumbuka zaidi matukio gani ya rais wa Tanzania kwa mwaka 2018?

Mwaka 2018, umefikia ukingoni na Rais John Pombe Magufuli amekuwa na mwaka wenye matukio tele ya kukumbukwa, je wewe utamkumbuka zaidi kwa lipi?

Mwezi huu wa Disemba, amepokea ndege ya tano toka alipoingia madarakani miaka mitatu iliyopita. Katika hafla ya mapokezi iliyofanyika kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, furaha ya rais Magufuli ilikuwa iwazi.

Akikamatana mkono na Waziri Mkuu wake, Kassim Majaliwa walisakata rhumba kabla ya kwenda kupiga ngoma. Ilikuwa ni tarehe 23 na yalikuwa ni mapokezi ya Airbus Airbus 220 - 300.
Kati ya ndege saba ambazo serikali ya Magufuli iliazimia kununua, tatu ni ndogo aina ya Bombardier Q400 ambazo zote zimeshawasili Tanzania na zinafanya kazi, na mbili ni za masafa ya kati aina ya Airbus amabayo moja imeingia mwezi huu na nyengine moja inatarajiwa kuingia mapema mwakani.
Ndege mbili ni kubwa na za masafa marefu aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, tayari moja imewasili mwezi Juni mwaka huu na ya pili inatarajiwa kuingia Tanzania 2020.
Wakati akiipokea ndege hiyo kubwa Magufuli alisema: "Tumefufua ATCL kurejesha heshima ya nchi, ilikuwa aibu kutokuwa na ndege kwa nchi kubwa kama Tanzania ... Tangu tumeongeza ndege 3 mpya aina ya Bombardier Q400 biashara ya ATCL imeongezeka, Shirika letu lilikuwa linasafirisha abiria 4,000 tu kwa mwezi lakini sasa linasafirisha abiria 21,000 na ndege zinatua katika vituo 12."
Magufuli pia alitupilia mbali kuwa ununuzi wa ndege hauna manufaa kwa watu walio wengi: "Ndege zote hizi tumenunua kwa fedha zetu wenyewe, hatujakopa kwa mtu...Madai kuwa Watanzania wengi hawafaidiki na ndege hayana msingi. Wapo wengi wanaohitaji ndege bei ilikuwa juu."

Ununuzi wa korosho

Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi, rais Magufuli alitiangaza Novemba 12 kuwa Serikali kupitia Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) itanunua korosho zote kutoka kwa wakulima.
Hatua hiyo ilifuata baada ya serikali kutoafikiana na wafanyabiashara ambao hawakufikia kiwango cha shilingi 3,000 kwa kilo.
Mzozo ulianza baada ya wakulima katika mikoa ya kusini kugomea bei kati ya Sh shilingi 1,900 hadi 2,700 kwa kilo. Serikali iliungana na wakulima na baada ya kukutana na waafanyabiashara kwenye kikao ambacho rais Magufuli alishiriki bei ya kuanzia shilingi 3,000 'ikakubaliwa', lakini utekelezaji wake haukufanikiwa.
Mwaka jana kilo ya korosho ilifikia kuuzwa mpaka kwa shilingi 5,000 kwa kilo.
Baada ya amri ya rais, wanajeshi walianza kutekeleza 'Oparesheni Korosho' na walielekea mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma kulinda maghala na kusafirsha zao hilo.
Sakata hilo pia liliwang'oa uongozini waziri wa kilimo Charles Tizeba na waziri wa biashara Charles Mwijage.


korosho

Kumekuwa na maoni tofauti juu ya hatua hiyo ya kulihusisha jeshi, wapo wanaosifu na wengine wakikashifu na kulaumu.
Mnamo mwezi Juni mjadala mkali ulizuka nchini Tanzania kuhusu mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2018 /2019 katika zao la korosho. Mapendekezo hayo ni pamoja na kuondolewa kwa ruzuku ya asilimia 65 iliyokuwa inaenda kwenye Mfuko wa Maendeleo wa Korosho na badala yake, iende kwenye mfuko mkuu wa serikali.
Ingawa mapendekezo hayo yalipita, wabunge wa mikoa ya kusini bila kujali tofauti za kisiasa waliungana kupinga. Walifikia hatua ya kutishia kuandamana.
Rais Magufulia akajibu kuwa laiti wangeliandamana na kuzua ghasia basi angewatuliza kwa kutumia vyombo vya usalama.
Alimwambia waziri mkuu Majaliwa ambaye anatokea Lindi kuwa angalianza na shangazi yake kama maandamano yangefanyika.

No comments